Jinsi ya kukabiliana na athari za kiafya za kukaa muda mrefu

Jamii Africa
USA, New Jersey, Jersey City, Man watching tv at home

Imethibitishwa bila shaka kwamba kukaa muda mrefu kwenye magari, ofisini au kwenye viti kunasababisha matokeo hasi kwa afya.  Tabia hiyo ya kukaa muda mrefu inahusishwa na kupata uzito uliopitiliza, magonjwa ya moyo, kisukari na magonjwa mengine yasiyoambukiza.

Lakini utafiti mpya uliotolewa hivi karibuni, unatoa hamasa kwamba baadhi ya shughuli za mwili ikiwemo njia rahisi za kuimarisha misuli zinaweza kumsaidia mtu kukabiliana na athari za kiafya za kukaa muda mrefu.

Katika utafiti huo uliochapishwa kwenye jalida la BMC Medicine, watafiti wakiongozwa na Carlos Celis-Morales kutoka Chuo Kikuu cha Glasgow walichambua data za watu 400,000 wenye umri wa kati nchini Uingereza.

Watafiti hao walifanya ulinganifu wa ripoti za watu waliofanya  shughuli za mwili kama mazoezi na muda waliotumia kuangalia runinga au kompyuta. Ili kupata  vipimo halisi vya mazoezi waliyofanya watu hao, wanasayansi walifanya jaribio la uwezo wa kushika vitu ambapo watu walibana kifaa maalum kupima nguvu ya misuli.

Celis-Morales anasema jaribio la misuli ni rahisi kwasababu linasaidia kufahamu kwa kiasi gani mtu  yuko hai na nguvu ya misuli yake kuhimili mabadiliko ya mwili wakati amekaa.

Wamebaini kuwa watu ambao wana misuli dhaifu wana uwezekano wa asilimia 31 ya kufa mapema kama watatumia saa mbili mbele ya runinga, ukilinganisha na watu wenye misuli imara ambao wanatumia muda kama huo. Pia watu hao wana hatari kwa asilimia 21 kupata magonjwa ya moyo na 14% kupata kansa ukilinganisha na wale wenye misuli imara.

 Kukaa muda mrefu ni hatari kwa afya yako

Kwa muktadha huo, kwa kila masaa 2 ambayo watu wenye misuli dhaifu wanatumia mbele ya runinga au kompyuta, hatari ya kufa kwasababu yoyote inaongezeka mara mbili kuliko wale wenye misuli imara.

Habari njema ni kwamba nguvu ya misuli inaweza kuimarishwa kwa mafunzo ya kupunguza uzito na kufanya mazoezi ya mwili, amesema Celis-Morales. “Ujumbe wa jumla ni kwamba haijalishi kwa muda gani umekaa au kuangalia runinga hata kama uko imara na hai kimwili,” amesema. “Ikiwa utatembea, kusimama na kujinyoosha hautapata athari sawasawa na mtu ambaye amekaa muda wote bila kupasha misuli.”

Ni muhimu kufahamu kwamba kukaa muda mrefu sio jambo jema kiafya, amesema; ukilinganisha na watu ambao hawakaii muda mrefu. Watu ambao ni wavivu wana viwango vya juu kupata magonjwa na kufa mapema. Lakini kwa wale ambao wanakaa muda mrefu na kuwa hai wanaweza kupunguza athari za kiafya.

Hata hivyo, hilo sio kosa letu. Kadiri tunavyoondoka kwenye mtindo wa maisha ya zamani ya kilimo na kuingia kwenye shughuli za ofisini na usafiri wa kisasa hadi kwenye mfumo wa kila siku wa maisha, chakula, kazi na burudani tunajenga kipaombele kimoja kwenye akili; faraja. Wazee wetu walitumia muda wao mwingi kutembea, lakini maisha ya kisasa yanakulazimisha kukaa kukaa muda mrefu.

Lakini bado tuna wajibu wa kufanya kuhakikisha miili yetu inaendelea kuwa hai na kuepukana na magonjwa yasiyo ya lazima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *