Kwanini wanawake hupata msongo wa mawazo kwa kiwango kikubwa kuliko wanaume?

Jamii Africa
Black woman frowning with head in hands

Kama ambavyo imekuwa ikielezwa na baadhi ya vyombo vya habari, wanawake wapo kwenye nafasi ya kupata msongo wa mawazo kwa kiasi kikubwa kuliko wanaume. Pia kiwango chao cha kupata matatizo ya kiafya au kujiua ni kikubwa mara tatu ya kile cha wanaume.

Utofauti huu kati ya jinsia hizi mbili bado haupo bayana, baadhi ya watu wanaamini takwimu hizi zimeongezwa chumvi kwasababu tu wanaume ni viumbe “dhaifu” hivyo ni rahisi kwa wao kuonesha dalili hizo. Hata hivyo baadhi ya tafiti zinaonesha kwamba madai haya ni ya kweli, kama hizi zifuatazo:

1. Utofauti wa homoni huchukuliwa kama kigezo kikubwa. Ukilinganisha na wanaume, wanawake hukumbana na matatizo mengi katika viwango vya homoni mwilini ambayo huusishwa na dalili za msongo wa mawazo. Mbali na matatizo mbalimbali ya hedhi, asilimia 15 ya wanawake hupata msongo wa mawazo baada ya kujifungua.

Msongo wa mawazo hujitokeza sana katika kipindi ambacho hedhi hukoma, ambapo melancholia ilibainika kuwa moja ya matatizo ya kiakili mpaka kufikia mwaka 1980. Pia wanawake wapo kwenye nafasi kubwa ya kupata matatizo ya upungufu wa homoni ya thyroid (tezi yake ipo kwenye shingo), ambapo mara nyingi huusishwa na msongo wa mawazo.

2. Kutokana na kigezo cha kimaumbile wanawake wapo kwenye nafasi kubwa ya kupata msongo wa mawazo kutokana na tafiti mbalimbali za mapacha wasiofanana, pia kutokana na historia ya familia.

3. Wanawake hujihusisha zaidi kwenye mahusiano binafsi kuliko wanaume na huathirika zaidi pale wanapovurugwa. Wanawake wengi walioolewa na wale ambao ni mama wa nyumbani wamekuwa na majukumu makubwa zaidi na kujikuta wanashindwa kuhimili majukumu ya kazi na familia, kama vile kutunza na kulea ndugu ambao ni wazee.

 

 Wanawake wenye umri kati ya miaka 25 mpaka 40 kiwango chao cha kupata msongo wa mawazo kimeongezeka mara nne zaidi ya wanaume.

Utafiti uliofanyika Ulaya kwenye nchi zaidi ya 30 na kuhusisha watu milioni 514 umebaini kwamba kiwango cha wanawake wenye umri wa kati kupata msongo wa mawazo kimeongezeka ndani ya miaka 40 kutokana na shughuli hizi. Wanawake wenye umri kati ya miaka 25 mpaka 40 kiwango chao cha kupata msongo wa mawazo kimeongezeka mara nne zaidi ya wanaume.

4. Wanawake huishi kwa miaka mingi zaidi kuliko wanaume na hii huusishwa na kukosa matumaini, upweke, hali mbaya ya kiafya na matatizo mengine ambayo husababisha msongo wa mawazo.

5. Wanawake ni wepesi sana kutafuta kuonana na wahudumu wa afya pale wanapojisikia kwamba hawapo vizuri kiafya tofauti na wanaume, hivyo ni rahisi kwa wao kugundulika wanapokuwa na matatizo ya kiafya. Pia kuna ushahidi kutoka kwa madaktari wa kike na wa kiume kuhusu wepesi wa kugundua hali ya msongo wa mawazo kwa wanawake zaidi kuliko wanaume kwa dalili zinazofanana.

6. Dalili za huzuni kwa wanawake ni kubwa mara nne zaidi ya ilivyo kwa wanaume, na matokeo yake huongezeka zaidi kadiri majira na nyakati zinavyobadilika. Mfano, Tromso mji uliopo Norway, huwa na karibu siku 50 kipindi cha baridi ambapo jua huwa halionekani kabisa.

Katika kipindi hiki watu huchoka sana na kiwango cha utendaji kazi hupungua. Pia kuna ongezeko kubwa la msongo wa mawazo hasa kwa wanawake. Ajali na mauzo ya dawa mbalimbali za usingizi huongezeka zaidi katika kipindi hicho.

Hata hivyo wanawake walio kazini na wale wasio na wenzi wapo kwenye nafasi kubwa si tu ya kupata msongo wa mawazo lakini pia magonjwa ya moyo, kansa ya matiti na kansa ya kizazi.

Pamoja na ushahidi uliotolewa hapo juu, bado tafiti zaidi zinahitajika juu ya nadharia za msongo wa mawazo kwa wanaume na wanawake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *