Mahakama Kuu yazuia utekelezaji wa kanuni za Maudhui Mtandaoni

Jamii Africa
  • Ni zile zinazowataka wamiliki wa blogu na runinga za mtandaoni kupata leseni toka serikalini
  • Wanaharakati wasema zinakiuka haki za msingi za binadamu

Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara  imetoa  zuio la muda  linalozuia matumizi ya Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni  ampaka kesi  ya msingi iliyofunguliwa na watetezi wa haki za binadamu itakaposikilizwa.

Kimsingi kanuni hizo zilipaswa kuanza kutumika Mei 5 mwaka huu, baadaya ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ilitoa wiki mbili kwa wamiliki wa blogu, majukwaa, redio na runinga za mtandaoni kuwasilisha maombi katika mamlaka hiyo ili kupata leseni ya kuendesha shughuli zao mtandaoni.

Hii inatokea kiwa imebaki siku moja kwa tarehe ya mwisho na iliyowekwa na TCRA kuwasilisha mambi ya leseni, Mahakama Kuu imetoa zuio hilo baada ya taasisi sita kuwasilisha mahakamani maombi ya kuzuia matumizi ya Kanuni hizo April 30, mwaka huu.

Taasisi zilizowasilisha maombi hayo mahakamani ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRD), Baraza la Habari Tanzania (MCT), Jamii Media, Chama Cha Wanawake Wanahabari Tanzania (TAMWA) na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Katika kesi ya msingi ya mapitio ya kanuni hizo, taasisi tajwa zimewashitaki  Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika maombi ya msingi taasisi hizo zinaiomba Mahakama Kuu kufanya mapitio ya kanuni hizo kwa kigezo kwamba Waziri ametumia nguvu ya kisheria nje ya mamlaka yake ( Ultra vires). Pia kanuni hizo zinakiuka haki ya usawa  katika matumizi ya mitandao ya kijamii bila kuwekewa vikwazo vinavyoathiri kundi fulani la watu.

Maombi hayo pia yamejikita kupitia kanuni hizo kwasababu zinapingana na haki ya kujieleza ( Freedom of exepression) haki ya kusikilizwa( rights to be heard) , na haki ya usiri ( Privacy rights) ambazo zote kwa pamoja zinawahusu moja kwa moja watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Baada ya zuio hilo la Mahakama Kuu kanda ya Matwara, imepanga kusikiliza  tena kesi ya msingi Mei, 10 2018.

 

Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni

Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni (Online Content Regulations) zilipitishwa na serikali Februari mwaka huu ili kufanya kazi sambamba na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, ambayo imekuwa ikilalamikiwa kwa kuminya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni.

 Kwa mujibu wa Kanuni hizo ili mtu akubalike kutoa huduma ya blogu, jukwaa, redio na runinga za mtandaoni, muombaji atalazimika kujaza fomu inayoelezea gharama tarajiwa za uwekezaji, idadi ya wakurugenzi na wafanyakazi na wana hisa wa jukwaa/blogu husika . Pia kila mwana hisa anapaswa kuainisha mtaji aliochangia kwenye huduma husika, tarehe ya kuanza kufanya kazi na mipango ya baadaye ya ukuaji wa blogu.

Pia wamiliki wanapaswa kulipa kiasi kisichopungua milioni 2 ili apate leseni, jambo ambalo limepingwa na wadau wa habari nchini wakidai ada hiyo ni kubwa na inalenga kuzuia upatikanaji wa habari kwa wananchi kwasababu wamiliki wengi hawana hicho kiasi.

Licha ya mamlaka husika kutoa kibali au leseni ya kuendesha blogu, pia ina nguvu kisheria kunyang’anya kibali/leseni ikiwa blogu itachapisha maudhui yanayodhaniwa ‘ kusababisha au kuhatarisha amani, kuchochea machafuko au uhalifu’ au ‘yanatishia usalama wa taifa au afya na usalama wa umma’.

                         Watumiaji wa simu janja nao watakasa taarifa

 

Waliopewa mamlaka ya kusimamia maudhui ya mtandaoni ambao ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) watakuwa na uwezo pia wa kuwalazimisha wamiliki wa blogu au tovuti kuondoa maudhui yanayodhaniwa kuwa hayafai ndani ya saa 12 na kama hawajatimiza maagizo hayo wanaweza kulipa fidia isiyopungua milioni tano  au kifungo kisichopungua mwaka mmoja jela.

Tangu zilipopendekezwa mwaka jana, wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu ikiwemo Mwanzilishi wa JamiiForums, Maxence Melo walijitokeza na kuhoji baadhi ya vipengele ambavyo vilionekana kukiuka faragha za watu, kuminya uhuru wa wananchi kujieleza na kutoa maoni.

Kanuni hizo zitaithiri JamiiForums kwasababu watumiaji wake watatakiwa kutumia majina halisi na siyo ilivyo sasa ambapo mtu ana uamuzi wa kutumia jina lolote. JamiiForums ilifanya hivyo ili kulinda faragha za watumiaji wake na kuongeza uhuru kujieleza.

Haya yote yanatokea Tanzania, ambako juhudi mbalimbali za kuinua teknolojia ya mawasiliano na habari zinaendelea ili kushindana na nchi jirani za Afrika Mashariki kama Kenya.

“Masharti ya usajili na ada yanaonekana kuwa mzigo mkubwa kwa waanzilishi wa blogu na runinga za mtandaoni, hatimaye itakamwamisha mchakato wa kuinua uhuru wa habari nchini”, alisema, Angela Quintal, Mkurugenzi wa Kamati ya Afrika ya Kuwalinda wanahabari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *