Mambo 5 ambayo mtu hawezi kukwepa muda mfupi kabla ya kufa

Jamii Africa
Profile of a father sitting beside his son lying on the bed

Una majuto yoyote? Naamini watu wengi wana majuto (regrets) kwasababu wamefanya baadhi ya maamuzi yenye matokeo hasi au hawakufanikiwa kupata yale waliyoyatarajia yangetokea katika maisha yao.

 Lakini majuto yetu yanapata nguvu wakati tunakaribia mwisho wa maisha yetu hasa siku chache kabla ya kifo.

Kwa miaka mingi, Bronnie Ware,  Muuguzi na Mshauri wa masuala ya afya katika nchi ya Australia, amekuwa akifanya kazi katika kitengo cha Kuwapunguzia wagonjwa maumivu huku akijikita kuwasaidia wale ambao wana hali mbaya na wanakaribia kufa. 

Wagonjwa wake walikuwa wazee wenye matatizo makubwa ya kiafya wakisubiri kufa. Alitumia muda mwingi kuwapa ushauri, faraja na kuwapunguzia maumivu ya akili na mwili ambayo yanakuja mtu anapokikabili kifo.

 Kifo sio jambo la kufurahisha na kukubalika kwa watu wengi; tunapendelea kutofikiri au kuzungumzia. Habari ya kusikitisha ni kwamba kila mtu atakufa kwa wakati wake.

 Kujua unaenda kufa wiki chache zijazo ni jambo linaloumiza sana. Bronnie amekuwa akishuhudia hali wanayoipata wagonjwa wake muda mfupi kabla ya kufa ambapo wengi wao wanajikana, halafu wanapata hofu, hasira, majuto, kujikana zaidi na mwisho kukubali hali halisi ya kinachoenda kutokea.

Kama sehemu ya kazi, Bronie amekuwa akiwauliza wagonjwa wake kuhusu majuto waliyonayo katika maisha na kama kuna jambo ambalo wangelifanya kama wangepewa nafasi ya pili ya kuishi.

Katika majibu yote aliyoyapata kutoka kwa wagonjwa wake, aligundua majuto 5 ambayo yamekuwa yakijurudia sana. Yafuatayo ni majuto ambayo wagonjwa wanajutia sana muda mfupi kabla ya kufa:

 

1) Natamani  ningetimiza ndoto na malengo yangu na sio maisha ambayo watu wengine wangetarajia kutoka kwangu

Kwa mujibu wa Bronnie, anasema hili ndio juto la kawaida kwa watu wengi. Watu wakifahamu kuwa maisha yao yanafika mwisho, ni rahisi kuangalia nyuma na kukumbuka ndoto na malengo yote ambayo hawakutimiza lakini hawana ujasiri tena wa kutekeleza.

 Anaeleza kuwa kushindwa kutimiza malengo kwa watu hao ni kwasababu waliwekeza nguvu zao kutekeleza matakwa ya watu wengine- kawaida ni familia, marafiki na jamii.

 Mmoja wa wagonjwa wake aitwaye Grace alimwambia Bronnie anaahidi kutekeleza ndoto zake zote na kuishi maisha yake kwa utoshelevu bila kujali watu wanasema nini.

 Bronnie anasema kwa muda mrefu ndoa ya Grace haikuwa na furaha, na mume wake alikuwa akitibiwa nyumbani. Majuto makubwa ya Grace ni kuwa hakuwa na uwezo wa kuzifikia ndoto zake kwasababu ya kumuuguza mume wake kwa muda mrefu.

 

 2) Natamani ningeimarisha mahusiano ya familia

 Kwa mujibu wa Bronnie anasema majuto ya aina hii yamemkuta kila mwanaume mgonjwa aliyemuuguza huku wanawake wakiwa wachache. Wengi wao walikuwa wakifanya kazi kwa saa nyingi na kuzisahau familia zao.

 Majuto yao yalikuwa ni kukosa ukaribu kwa watoto na wake zao. Walipouliza nani atafanya tofauti ikiwa atapata nafasi ya pili, majibu yalishangaza sana. Wengi wao waliamini kuwa wangerahisisha maisha na kufanya maamuzi sahihi ya kutumia muda mwingi na familia.

Kwa jinsi hiyo tunaweza kuyapa maisha nafasi ya kupata furaha na kuimarisha upendo na amani kwa watu walio karibu yetu.

 

 3) Ningekuwa na ujasiri wa kuelezea hisia zangu na kuongea kile ninachokiamini

 Bronnie anaendelea kusema kuwa wagonjwa wake wengi waliamini kuwa hawaheshimu hisia zao na hawakuongea yale waliyoyaamini kwasababu walitaka kudumisha amani na watu.

 Wengi wao walichagua kutokabiliana na hali ngumu, watu hata kama walidharirishwa. Ili kutuliza hasira, walijijengea maumivu na uchungu kati mioyo yao na mwisho yakaathiri afya zao. Jambo baya zaidi ni kukumbatia vinyongo na uchungu ambapo huathiri hisia na kuzuia mafanikio yetu.

Kuzuia aina hii ya majuto katika maisha ya baadaye ni muhimu kuelewa kuwa busara na kukabiliana na matatizo ni sehemu ya kuimarisha mahusiano na kutengeneza furaha.

 Kwa kuongea yale yaliyopo moyoni tunatoa hisia za kweli na kupunguza hatari ya kujenga machungu na majuto ambayo yanaweza kutuumiza.

 

4) Natamani ningekaa karibu na marafiki zangu

Bronnie amegundua kuwa wagonjwa wake wanakosa ukaribu na rafiki zao na wanajuta kwanini hawakutumia muda mwingi na marafiki hao kama ilivyowapasa.

 “Kila mmoja anawakumbuka rafiki zake wakati wa kufa”, anasema John-Paul Iwuoh, Mtaalamu na Mshauri wa biashara na ujasiriamali.

 Wakati afya na ujana ukiteteleka na kifo kinakaribia, watu wanatambua kuwa urafiki na baadhi ya watu ulikuwa na thamani kuliko utajiri na mafanikio. Bronnie anaongeza kuwa yote hayo yanatokea wakati wa mwisho wa safari ambapo mtu hukumbuka upendo na mahusiano mazuri.

 Tunaishi katika dunia yenye shughuli nyingi na kutusahaulisha kuwa tuna marafiki ambao wanaweza kutupatia furaha na thamani katika maisha.

 

5)Natamani ningeishi kwa furaha

Wagonjwa wa Bronnie hawakutambua hadi walipofika mwisho wa maisha yao kuwa furaha ni uchaguzi. Wanatamani wangefahamu kuwa furaha sio jambo la kukimbilia na kujipatia utajiri, kukubalika katika jamii na masumbufu ya maisha.

Wakiwa kwenye vitanda vya mauti, wagonjwa hao wanatambua kuwa wangechagua furaha bila kujali hali za maisha- utajiri au umaskini.

John-Paul Iwuoh anasema wakati mwanadamu akiwa mzima na mwenye afya anawekeza nguvu zake kujipatia vitu, utajiri, hadhi, madaraka na mafanikio. Na tumekuwa tukiamini kuwa hivi vitu vitatuletea furaha.

 Walipoulizwa wanaweza kufanya tofauti, hili ndilo jibu walilolitoa: Jifunze kuridhika na kukubali vitu vizuri katika maisha yako. Na hii ndio njia ya kweli ya kupata furaha.

  

Inawezekana kuishi bila kuwa na majuto?

John-Paul Iwuoh anasema hakuna mwanadamu aliyekamilika, na anapata mashaka juu ya ‘maisha ya ukamilifu’. “Natumaini kila mmoja awe na majuto katika siku yake ya kufa. Lakini nafikiri jambo la muhimu ni kuwa na majuto machache kadiri tuwezavyo”.

Hata hivyo, Iuoh anasema kufa ukiwa na majuto machache ni kuishi maisha kwa kiwango kinachostahili na kutambua kuwa unaweza ukafa wakati wowote. Katika yote hakuna anayefahamu siku ya kufa kwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *