Programu za jinsia shuleni kuvunja mnyororo wa ukatili kwa watoto Dar

Jamii Africa

Imeelezwa kuwa watoto yatima wako katika hatari kubwa ya kukumbwa na ukatili wa kijinsia na kuathiri ustawi wa maisha yao kiuchumi na kielimu.

Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ni suala zito la haki za binadamu, jamii na afya ya jamii nchini Tanzania kama ilivyo katika nchi nyingi duniani. Vitendo hivi vinamomonyoa msingi imara ambao watoto wanahitaji ili wawe na afya bora na maisha yenye tija, na vinasigana na haki ya msingi ya watoto ya kuishi salama utotoni.

Kwa mujibu wa Ripoti ya utafiti wa  Ukatili Dhidi ya Watoto Tanzania ya mwaka 2009 iliyotolewa na shirika la Watoto Duniani (UNICEF), yatima wako katika hatari zaidi ya kukumbwa na ukatili kuliko wasio yatima kutokana na kukosa malezi ya familia ambayo ndiyo msingi wa ukuaji wa mtoto.

“Ukatili wa kijinsia uliowakumba watoto kabla ya miaka 18 ni asilimia 36 ya wasichana waliokuwa yatima ukilinganisha na asilimia 25 ya wasichana ambao hawakuwa yatima, na ukatili wa kiakilia utotoni uliwakumba wasichana yatima asilimia 31 ukilinganisha na asilimia 21 ya wasichana wasio yatima,” imeeleza sehemu ya ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inaelezwa kuwa ukatili unawakumba zaidi watoto yatima ni ule wa kiakili na kimwili ambapo asilimia 9 ya wasichana na asilimia 14 ya wavulana nchini Tanzania wamewahi kufanyiwa ukatili wa kiakili na kimwili kama kupigwa na kutukanwa.

Kulingana na Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009, mtoto anahesabika kuwa ni yatima endapo atafiwa na mzazi mmoja au wote wawili. Kimsingi anakosa matunzo au upendo wa mzazi mmoja au wote wawili ambapo inaweza kuwa ni changamoto katika ukuaji wake hasa katika upatikanaji wa elimu.

              Watoto bado wako kwenye hatari kubwa ya kufanyiwa ukatili

 

UNICEF katika ripoti hiyo, inaeleza kuwa umaskini, mmonyoko wa maadili na ongezeko la magonjwa ni baadhi ya sababu zinazoshamirisha watoto yatima katika jamii.

“Yatima wako katika hali hatarishi zaidi. Umasikini, kupanuka kwa miji, kumomonyoka kwa maadili na desturi za familia, na athari za janga la UKIMWI/VVU vinaashiria kwamba watoto ambao hawako katika utamaduni wa kuishi kifamilia na kijamii wako katika hali hatarishi ya kukumbwa na ukatili,” inafafanua ripoti hiyo.

Wavulana waliopoteza mzazi mmoja hasa mama, ndiyo wako katika hatari ya kufanyiwa ukatili na mama zao wa kambo kwa hufanyishwa kazi ngumu na wakati mwingine hunyimwa chakula na sehemu ya kulala.

Ripoti ya UNICEF inafafanua zaidi kuwa, “Wavulana waliopoteza mama zao kabla ya kufika umri wa miaka 18 walikumbwa zaidi na ukatili wa kiakili kuliko wale wasio kuwa yatima (asilimia 44 ya wavulana yatima ukilinganisha na asilimia 26 wasiokuwa yatima)”.

Matokeo ya utafiti huo ni kielelezo tosha cha hali halisi ya ukatili dhidi ya watoto yatima  iliyopo katika jamii hasa katika jiji la Dar es Salaam, ambapo katika mitaa na barabara kuu hutaacha kuwaona watoto wadogo wakizurula na kuomba fedha kwaajili ya kujikimu.

Ili kupambana na ukatili dhidi ya watoto yatima serikali imeshauriwa kujumuisha ujumbe wa kuzuia ukatili wa kijinsia na sehemu salama kwenye programu za shule kuzungumzia jinsia, afya ya uzazi, na maendeleo ya jamii.

Hata hivyo,  ili mapambano yafanikiwe imetakiwa  kupanua ulinzi stahili wa kisheria kwa watoto na adhabu za kisheria kwa wakosaji; kuendeleza jitihada zilizopo kwenye Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi kitaifa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *