3/4 ya Wanafunzi S/M Pamba ‘B’ wanaketi sakafuni

Jamii Africa

JUMLA   ya  wanafunzi 630, sawa na robo tatu ya wananafunzi   832   wanaosoma katika  shule  ya  msingi Pamba B Jijini  hapa  wanaketi  sakafuni  kutokana na upungufu mkubwa  wa madawati  unaoikabili shule hiyo.

Taarifa hiyo ilitolewa  0ktoba 10  mwaka huu na Mwalimu  Mkuu  wa  shule hiyo, Sophia  Iboni  wakati  akipokea  msaada wa madawati 40  yaliyotolewa  na Mfuko  wa  Pensheni  kwa Mashirika ya Umma (PPF).
“…Kwa  kweli tunaushukuru  uongozi wa PPF kwa msaada  huu wa madawati 40; ingawa  kweli bado tunaupungufu  mkubwa  kwa sababu   tunayo  madawati 102  tu!” alisema mwalimu  Iboni.
Picha toka Maktaba
Kwa   mujibu wa  mwalimu Iboni, zaidi  ya  wanafunzi 630  wanaketi  sakafuni  shuleni hapo.Mwalimu  Iboni   alifafanua  kwamba  shule hiyo  inakabiliwa na upungufu wa  madawati   127.
Alisema pia kwamba shule hiyo  inakabiliwa  na uhaba  mkubwa wa walimu wa kike. Aliendeea  kufafanua kwamba  shule hiyo ina jumla ya walimu 17, wote  wa kike.
“ Ombi  letu kwa  wadau  na taasisi  zingine ni kwamba bado tunahitaji msaada zaidi  a madawati” alisema  Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Mashaka Baltazar  wakati  akimkaribisha Meneja  wa PPF kanda ya ziwa.
Baltazar  aliyataja matatizo mengine  yanayoikabili  shule hiyo  kwamba ni  upungufu  wa matundu ya choo. Mwenyekiti huyo   alisema  shule hiyo  ina  matundu manne  tu ya  choo; matundu ambayo  uwiano wake  hauendani na wingi  wa  wanafunzi.
“ Tumesikia  maombi yenu, na kikubwa  ni kwamba  bado  shule hii  inahitaji  madawati zaidi. Hata  hivyo, nitalipelekeka  ombi hili  katika Menejimenti ya Mfuko” alisema  Meneja  wa PPF  kanda  ya ziwa,  Meshach  Bandawe  na kuongeza  kuwa  amekabidhi msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi  wa  Mfuko huo.
Alisema ni sera  ya  PPF kutoa misaada  katika  jamii; lengo likiwa ni kusaidiana na serikali kuu. Bandawe  alisema madawati yaliyotolewa yana thamani ya shilingi milioni 2.1.
Habari hii imeandikwa na Juma Ng’oko, Mwanza
1 Comment
  • Hapo ndiyo utaona serikali ya kiwewe imeshindwa kuwa na maono kwa maendeleo ya taifa inaenda kwa upepo,Tz si nchi ya kufanya Ukuajia kiuchumi(Economic Growth)kwani ni hatari kwa taifa la kesho mfano,wanafunzi 300 wanaokaa chini au 300 walio kosa mlo wa mchana shule wakakimbia vipindi,au waliochoka kutembea kilomita 18 kwenda shule wakafeli darasa la saba,halafu wazazi wao hawana pesa ya kuwa endeleza na sekondari,inabidi waishie kwenye ajira mbaya za umalaya,uuzaji mifuko,uuzaji baa na migahawa,migodini n.k halafu wanaishia kufariki,kupata magonjwa hatari,kubakwa n.k kisa ni serikali imeshindwa fanya elimu ya sekondari bure na pili hakuna mipango ya kuwapeleka waliofeli ktk vyuo vya ufundi wasome bure,hapo kuwapotezea ramani ya masha watoto wasio na hatia ni uhaini serikali inastahili kufunguliwa mashitaka makubwa tu.

    Nachotaka kusema kwanini tusi thibiti idadi ya watu kwa sera nzuri?halafu tufanye Maendeleo kiuchumi yani ECONOMIC DEVELOPMENT ambapo ni kuongezeka kwa kiasi na ubora wa huduma za kijamii,Mfano kuloko kujisifia umejenga shule za kata 4000 zisizo na walimu wakutosha,madawati,maabara n.k jenga shule 2000 zenye walimu wa kutosha,madawati na maabara n.k.

    Serikali yetu inafanya vitu kuridhisha wahisani ambao pia ndiyo waporaji rasirimali zetu pitia ukoloni mamboleo,haiwezekani mkoa una dhahabu au Tanzanite au Misitu ya mbao n.k halafu hapohapo wanafunzi wanakaachini huku mbao zinavunwa na kuuzwa nje kama Iringa ilivyo,ni aibu serikali kuwa kichwa cha mwendawazimu.Ila mimi naamini malipo yao wahuni ni moto wa milele tu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *