Mzimu wa Richmond waendelea kuliumiza taifa

Jamii Africa

KASHFA ya Richmond-Dowans haionyeshi dalili zozote za kumalizika wakati kampuni ya kimarekani (Symbion Power) imeanza kuzalisha umeme.

Sehemu kubwa ya Tanzania inajitahidi kukabiliana na mgawo wa umeme unaochukua hata saa 16 kwa siku wakati serikali inajaribu kutatua mkanganyiko huo uliotokana na kashfa hiyo ya kuingizwa kwa mitambo ya umeme ya Richmond kwa ‘bei mbaya.’

Kampuni ya nishati ya Marekani, Symbion Power sasa imenunua mitambo hiyo ambayo imekuwa haifanyi kazi tangu Agosti 2008. Kiwango chake cha juu za uzalishaji ni megawati 120 na Tanzania inahitaji kiasi cha megawati 350.

Watanzania wanashuku sababu za kuwepo kwa mgawo wa umeme na hawaamini kwa haraka maelezo ya serikali kuwa chanzo ni kukarabati mashine katika mitambo ya umeme inayomilikiwa na kampuni ya Songas, hasa kwa sababu kina cha maji ni kikubwa katika uzalishaji wa umeme kwa maanguko ya maji.

Symbion Power haikueleza ni kiasi gani italipa kwa kununua mitambo hiyo iliyopo Ubungo lakini wataalamu katika sekta ya nishati wanasema ni kiasi cha dola za Marekani milioni 70.

Symbion tayari imekuwepo nchini iliweka miundombinu ya kusambaza umeme, sehemu kubwa ikilipiewa na Millenium Challenge Corporation ya Marekani.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Symbion, Paul Hinks, alisema majadiliano na Dowans yalikuwa na changamoto nyingi, akakubali kuwa taarifa za awali zilifanya Symbion ifanye ukaguzi wa kina kabla ya kuendelea na mpango huo.

Balozi wa zamani wa Marekani Joseph Wilson ambaye, pamoja na mkewe, ofisa wa zamani wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA). Valerie Palme Wilson, anaonyeshwa katika filamu ya Hollywood katika ushindani kisiasa na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Marekani, Dick Cheney, analeta ushupavu kiasi chake kama mwenyekiti wa Symbion Power Africa.

Wilson pia ni mkurugenzi wa Jarch Capital,, ambao hivi sasa iko katika shughuli pevu ya kununua maeneo makubwa ya ardhi nchini Sudan Kusini.

Vyanzo vya habari vinasema shirika la umeme nchini, Tanesco ilitaka kununua mitambo hiyo lakini serikali ikaikatalia kwa sababu ambazo bado hazijaelezwa.

Balozi wa Marekani nchini, Meja Jenerali Mstaafu Alfonso E. Lenhardt, alibariki mpango huo. Symbion imetoa taarifa kuwa mtambo huo uko katika hali nzuri, licha ya kuwa hautumiki kwa muda mrefu, na imekubali kutoa umeme wa bure kwa Tanesco wakati inaendelea na zoezi la kuanza tena kuitumia na kuunganisha na gridi ya taifa.

Tanesco katika hali ya kutatanisha ilifikia mkataba wa kutoa umeme wa dharura na Richmond (Development Company) mwaka 2006 baada ya ukame kusababisha upungufu mkubwa wa umeme wa maji.

Baadae Richmond ikaonekana haiwezi kuleta umeme, hivyo ikatoa mkataba huo kwa Dowans Holdings kwa ushawishi wa mawaziri. Richmond ikauza hisa zake (katika mradi huo) kwa Dowans, ambaye mwenye hisa wake mkuu ni raia wa Oman, Brigedia Jenerali Mstaafu Sulaiman Mohamed Yahya al-Adawi.

Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wawili walijiuzulu Januari 2008 kutokana na kufichuliwa kwa uhusika wao katika kufikia mkataba huo, baada ya uchunguzi wa Kamati ya Bunge.

Richmond ilipata kandarasi hiyo katika ushindani na makampuni ya umeme yenye hadhi, licha ya kutokuwa na usajili kamili kama biashara au kuwa na ujuzi wowote katika uzalishaji umeme.

Uchunguzi wa Bunge ulifikia tamati kuwa Richmond ilipewa kandarasi hiyo kutokana na upendeleo wa nguvu wa viongozi waandamizi serikalini.

HAKUNA MASHITAKA

Baada ya Symbion kuafiki kuanza kuwasha mitambo hiyo, maswali bado yanaulizwa kwanini ni machache sana kati ya mapendekezo 23 ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu suala la Richmond, yaliyopitishwa na Bunge, yametekelezwa.

Mapendekezo hayo ni pamoja na kutaka serikali kupitia upya mikataba kati ya Tanesco na Richmond-Dowans, Independent Power (T) Ltd, Alstom Power Rentals, Songas na Agrekko.

Pia ilipendekeza kufikishwa mahakamani kwa Richmond na wamiliki wake kwa kuiibia serikali.

Hakuna kati yao, akiwemo Naeem Gire, aliyetia saini mkataba na Tanesco, aliyeshtakiwa. Ripoti ya Kamati Teule iliainisha kuwa Tanesco inawajibika kwa mikataba yake na makampuni ya kufua umeme kulipia gharama za matengenezo, ubadilishaji vifaa, bima, kodi, huduma za kisheria na zaidi, iwe wanatoa umeme kwa gridi ya taifa au la.

Hali hii inaigharimu Tanesco dola milioni 1.3 kwa kampuni kwa mwezi, kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Vyazo vya habari ndani ya Chama Cha Mapinduzi vinasema kuwa licha ya kuwa ripoti hiyo ilikuwa ilishtua wengi, haikuivuruga CCM mradi Rais alikuwepo kuzuia kukinga kwa ufuatiliji kiutendaji, na kuzuia mashtaka yoyote.

Hata hivyo uchunguzi huo haukuwa umefurahisha hata kidogo uongozi wa CCM, na minong’ono ikaanza kuhusu nia halisi za wachunguzi Kamati Teule ya Bunge.

Wakasema kuwa Spika, Samuel John Sitta, na mwenyekiti wa Kamati Teule Harrison Mwakyembe walikuwa na nia ya kuanzisha chama kipya cha siasa na kuisuka taarifa ya uchunguzi kuendana na malengo yao hayo.

Wote wawili hata hivyo bado wako CCM. Sitta na Mwakyembe walifikiria kubadilisha utii wao kisiasa lakini iwe ni baada ya viongozi wa CCM, akiwemo Rais Jakaya Kikwete, kujaribu kuwaadhibu kwa kuruhusu uchunguzi huo ufanyike.

Ripoti pia ilipendekeza kusimamisha mkataba na Dowans. Hiyo ilifanyika Agosti 2008 lakini mzozo huo ukatinga baraza la usuluhisho la International Chamber of Commerce, ambako uamuzi wake ulikwenda kwa Dowans mwezi Novemba 2010 na serikiri ikaamriwa kulipa dola milioni 65 kwa kuvunja mkataba.

Kwa vile uamuzi wa ICC umeandikishwa rasmi nchini, Bunge haliwezi kujadili suala hilo. Mlango uko wazi, kwa wahusika wakuu wa mkasa wa Richmond-Dowans kutoka katika sakata hilo wakiwa wamelipwa ipasavyo na kuridhika, na kwa serikali kujitahidi kuondokana na jinamizi hilo.

Mweka Hazina wa zamani wa CCM na rafiki wa miaka mingi wa Rais Kikwete, Rostam Abdulrasul Aziz, anaaminika alikuwa ndiye mfadhili mmiliki wa Richmond, lakini hakuna uhakika ana hisa gani katika Dowans.

Al Adawi alisema mwezi Februari kuwa Aziz hakuwa mmoja wa wenye hisa na kuwa Al Adawi alimpa mamlaka ya uwakili mwaka 2005 kufuatilia suala hilo kwa niaba ya Dowans kwa sababu ‘ni rafiki yake wa miaka mingi na ana nguvu kuwakilisha kampuni yangu.’

Licha ya upinzani kuzuka karibu kila mahali, serikali italipa fidia ya Dowans, kwa mujibu wa vyanzo ndani ya CCM, ikitumia hukumu ya ICC kudai kuwa hakuna njia nyingine iliyobaki.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa serikali, Ludovick Utouh, aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ichukue jukumu la kulipa ‘baada ya kuingilia mkataba wa Tanesco na masharti yake.’

Migongano kati ya uongozi wa CCM na Sitta na Mwakyembe inaendelea.

Vyanzo vyetu ndani ya CCM vinasisitiza kuwa viongozi hao wawili walivunja maadili kwa kusimamia mashirika ya kitaifa dhidi ya makampuni binafsi ambayo yameisaidia CCM kifedha na hawawezi kutazamia fadhila wakati wamejaribu kuua bata anayetaga yai la dhahabu.

Kuna hisia kuwa sehemu ya pesa ya malipo kutokana na hukumu ya ICC itaingia katika makasha ya CCM kujazia gharama za kampeni za uchaguzi mkuu 2015.

Madai kama hayo kuhusu kampeni ya CCM ya uchaguzi mkuu 2005 katika uporaji wa dola milioni 116 kutoka akaunti ya madeni sugu ya nje, kashfa kubwa iliyotengezwa Benki Kuu.

Jina la Rostam Aziz (aliyekuwa mbunge wa Igunga na aliyejiuzulu ubunge hivi karibuni) pia liliibuka katika sakata hilo. TANESCO na wabunge wanaoitetea wanaamini kuwa imetumiwa tu katika mkabala wa kisiasa na kuwa vitendo vyote ambavyo imekuwa ikilaumiwa vinatokana na amri zilizotoka moja kwa moja kwenye Baraza la Mawaziri.

1 Comment
  • Kikombe cha Richmond-Dowans hakiwaepuki CCM, serikali na walio na madaraka katika ngazi zote za Tandagiza (Tanzania)

    Ingawa zahama ya matokeo hayo yote yanamuelemea Mtanzania maskini.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *