Balaa CCM: Basi la wajumbe lapata ajali na kuua dereva

Sitta Tumma

UCHAGUZI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), nafasi ya Uenyekiti mkoa wa Mwanza umeingia dosari baada ya basi walilokuwa wamepanda wajumbe kutoka Wilayani ya Kwimba mkoani hapa, kupata ajali mbaya ambapo wajumbe saba wamejeruhiwa vibaya, na dereva wa basi hilo amefariki dunia.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Bugongwa jijini Mwanza,  Jumanne saa 4:45 asubuhi. Chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa dereva wa gari aina ya fuso alipokuwa akigeuza katikakati ya barabara, ambapo dereva wa basi la Bedui alishindwa aliliparamia fuso hilo.

Basi lililopata ajali

Shija Malado ni shuhuda aliyenusurika katika ajali hiyo mbaya, alimtaja dereva wa basi hilo lenye namba za usajili T 853 BRB aliyefariki papo hapo kwa jina moja tu la Mihayo.

"Watu 10 waliopata ajali hiyo saba kati yao ni madiwani wa wilaya ya Kwimba. Mimi nimeruhusiwa muda mfupi baada ya kupata matibabu katika hospitali ya Bugando", alisema Malando.

Habari hii imeandikwa na Sitta Tumma – FikraPevu, Mwanza

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *