Bunda: Lishe duni yadaiwa kuwa chanzo cha kupungukiwa damu

Stella Mwaikusa

Imeelezwa kwamba kukosekana kwa lishe bora kwa  wajawazito na watoto katika wilaya ya Bunda,  ni chanzo cha makundi hayo kupungukiwa  damu.

Hayo yameelezwa na  mratibu wa afya ya mama na mtoto wilayani humo, Daines Lyimo, anasema hali hii inatokana na kuadimika kwa samaki ambao walikuwa ndio chakula na tegemo  kwa akinamama na watoto.

Daines anasema kwa sasa minofu ya samaki hupelekwa nje ya nchi na kuwaacha wakazi wa  Bunda, wakiwemo wajawazito na watoto kuishia kula viazi na vyakula vingine, ambavyo haviwezi kumsaidia mama na mtoto kuwa na afya njema pamoja na kinga bora ya mwili.

lISHE

Mratibu wa wilaya ya Bunda, Daines Lyimo akiwa na kaimu mkurugenzi wa Wilaya hiyo Charles Makame

Anasema kutokana na hali hiyo  wajawazito wengi  wanaojifungua wanakuwa na tatizo la upungufu wa damu na kulifanya  tatizo sugu kwa wilaya ya Bunda.

“Tatizo la upungufu wa damu kwa wilaya ya Bunda ni kubwa kwani ni 60% ya wajawazito wenye upungufu wa damu.” Anaeleza.

Daines anasema kila  wajawazito  10 wanaokuja kujifungua, basi wawili watakuwa na upungufu wa damu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *