Ipo Haja ya Kuliombea Taifa kuushinda Ufisadi – Mchungaji

Jamii Africa

MCHUNGAJI   wa  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri(KKKT) katika Usharika wa Inuka  lililoko kata ya  Mkuyuni  Jijini hapa, Jackob Kituu  ameshauri  Wakristo nchini  waache kula  angalau  kwa  siku kadhaa,   ili  pamoja na mabo mengine  wapate fursa nzuri ya kuliombea  taifa dhidi ya vitendo vya ufisadi pamoja na ushoga.

 

Mchungaji Kituu  alitoa  rai  hiyo wakati akihubiri  waumini wa kanisa hilo kwenye  maadhimisho ya  siku  kuu  ya Krismas, Jijini  hapa.

 

Vilevile,  mchungaji huyo  aliwataka  waumini  wa  kanisa hilo  ambao pia wamedhaminiwa nafasi za  viongozi  pamoja na watumishi  katika ofisi za umma  waache tabia ya kuomba  ama kupokea rushwa  kwa sababu vitendo hivyo vinamchukiza Mungu.

 

“ Kusema kweli  taifa  limefikia  hatua mbaya sana katika vitendo vya ufisadi;  na sasa Watanzania tunashauriwa na mataifa ya kigeni  eti  tukubaliane na ushoga. Ama kweli uovu  unaofanyika sasa hivi duniani unazidi  hata  uliokuwa ukifanyika nyakati  za Sodoma na Gomola na kuliko hata katika  siku za Nuhu” alisema Mchungaji Kituu .

 

Alisema kwamba ni vema  taifa likubali  hata kufa kutokana na umaskini, kuliko kukubaliana na masharti  ambayo yanayokiuka  uumbaji pamoja na sheria  za  Mungu.

 

“ Mimi nasema ni afadhali kufa maskini kulikoWatanzaia  kukubaliana na  ushoga; na nisema pia kwamba waumini  tusikualiane  na yeyote  anayetaka  kutuingiza majaribuni  juu  ya ushoga” alisema.

 

Kwa mujibu wa  mchungaji Kituu, ushoga ni hatua ya juu kabisa ya uovu  duniani; uovu  ambao umepewa  jina la utandawazi kwa kisingizio  cha  haki za binadamu.

 

“  Huwa inanishangaza sana  kwamba kila ninaposoma magazeti , kusiliza redio ama TV hukutana na majina   ya wakristo. Kwa  kweli  watu kama hao wanalitia doa kanisa la Mungu na wanapaswa   watubu!” alisema  mchungaji huyo.

 

Mchungaji Kituu  alisema ufisadi ni dhambi kama zilivyo  dhambi zingine  ambazo zimchukiza Mungu.

 

Alitumia fursa hiyo kuwataka  waumini wa  kanisa hilo kuchukia ufisadi  ambao alisema umeenea  hata katika baadhi ya nyumba za ibada nchini.

 

“ …ni aibu  kwa kiongozi au  mtumishi wa umma  kushiriki  katika kuomba na kupokea rushwa  huku akijua kuwa analipwa mshahara. Hivi ni kwa nini uombe rushwa; kwa nini uandike matumizi hewa  ofisini kwako! “ alihoji Kituu.

 

Aliwataka   waumini  wa kanisa hilo wawe mfano wa kuigwa katika jamii  na serikali  kwa kutenda mema siku zote; badala ya kusubiri nyakati za siku kuu pekee.

 

mwisho.

Na. Juma Ng’oko – Mwanza

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *